Mkutano huo ambao umetayarishwa na kundi la al Barak la Bahrain utajadili masuala mbalimbali ya kiuchumi katika mtazamo wa Kiislamu.
Zaidi ya wafanyakazi 700 wa benki kuu za nchi za Kiislamu, wakuu wa mabenki, wakurugenzi wa taasisi za kifedha, maulamaa na wataalamu wa masuala ya uchumi wa Kiislamu watashiriki katika mkutano huo.
Vilevile nakala ya kwanza ya insaiklopedia ya Fiqhi ya Uchumi iliyotayarishwa na kundi la al Baraka itazinduliwa katika mkutano huo. 830627