Licha kuwepo njama za Wazayuni za kupunguza idadi ya waumini wa Kipalestina katika Msikiti wa Al Aqsa katika Ijumaa ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, zaidi ya Waislamu laki moja walifanikiwa kufika katika msikiti huo na kusimamisha Sala ya Ijumaa.
Aghalabu ya waumini waliohudhuria Sala hiyo ya Ijumaa walitoka mji unaokaliwa kwa mabavu wa Quds na maeneo ya karibu. Aidha Wapalestina kutoka Ukingo wa Magharibi hasa wazee walifanikiwa kufika katika msikiti huo pamoja na kuwepo njama za utawala wa Kizayuni wa Israel kuwazuia kufanya hivyo.
Utawala haramu wa Israel kwa kawaida huwazuia watu walio chini ya umri wa miaka 50 kusali katika Msikiti wa Al Aqsa. 837851