IQNA

Uturuki mwenyeji wa kikao cha OIC kuhusu njaa Afrika

13:29 - August 10, 2011
Habari ID: 2168315
Kufuatia pendekezo la Uturuki, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imeitisha kikao tarehe 18 Agosti kwa lengo la kujadili kadhia ya njaa barani Afrika.
Duru za kidiplomasia zinasema Uturuki imetoa wito kwa OIC kuitisha kikao hicho maalumu ili kujadili hali ya njaa na ukame barani Afrika na hasa nchini Somalia.
Mapema Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Ahmet Davutoglu alikutana na Katibu Mkuu wa OIC Profesa Ekmeleddin Ihsanoglu ambapo walijadilia suala la misaada ya dharura kwa wanaokumbwa na njaa nchini Somalia.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran pia imetoa ombi la mkutano wa dharura wa OIC kujadili njia za kuwanusuru wanaokumbwa na njaa barani Afrika.
840629
captcha