Vitabu hivyo vimetarjumiwa na Sheikh Talib Khazraji. Mfumo wa kijamii katika Uislamu, swala katika Uislamu, masomo kutoka Nahjul Balagha, wilaya na al-Mahdi pamoja na masomo kutoka Qur'ani Tukufu ni baadhi ya vitabu vinavyoonyeshwa katika maonyesho hayo na jumuiya iliyotajwa.
Vitabu hivyo vimechapishwa na Kituo cha Kiislamu cha Brazil.
Mbali na Ureno kwenyewe, lugha ya Kireno pia huzungumzwa kama lugha rasmi nchini Brazil na nchi kadhaa za Kiafrika.
Maonyesho ya Kimataifa ya Qur'ani yanayoendelea mjini Tehran yamepangwa kukamilika tarehe 26 mwezi huu wa Agosti. 841737