Katika taarifa hiyo Ihsanouglu ameitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka ili kuingilia kati na kusimamisha jinai zinazofanywa na utawala huo dhidi ya Wapalestina wasio na wa kuwalinda.
Amesema mashambulio hayo yanayopelekea kuuawa na kujeruhiwa watu wasio na hatia wakiwemo wanawake na watoto wadogo, licha ya kuwa yanakiuka sheria za kimataifa pia yanavuruga uthabiti wa Mashariki ya Kati.
Katibu Mkuu wa OIC ametaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya utawala haramu wa Israel ili kuulazimisha kusimamisha mara moja mzingiro uliouwekea Ukanda wa Gaza. 848426