Sheikh Mahir Hamoud amesema kuwa Siku ya Kimataifa ya Quds ni hatua muhimu katika njia ya kuwatetea wananchi wanaokandamizwa mbele ya mabeberu kwa moyo uliojaa imani na yaqini kamili kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu SW itatimia.
Naye Ahmad Zein, Mwenyekiti wa Baraza la Maulamaa wa Lebanon amesema kuwa haifai katika kipindi hiki ambapo madola ya kibeberu yanauunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel na kuusaidia kwa hali na mali, kuwaacha peke yao wananchi wa Palestina.
Sheikh Ikrima Sabri, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Quds Tukufu amesema Siku ya Kimataifa ya Quds imehuisha kadhia ya Palestina katika nyoyo za vizazi vijavyo, kwa msingi huo kuna udharura wa kusisitiza juu ya umuhimu wa suala hilo kwa ajili ya kuweza kufikia lengo tukufu la kuikomboa Quds Tukufu. 849034