IQNA

Siku ya Quds yaadhimishwa kwa mara ya kwanza Tunisia

14:39 - August 27, 2011
Habari ID: 2177148
Watu wa Tunisia kwa mara ya kwanza mwaka huu wameadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds katika kile kilichotajwa kuwa ni matunda ya mapinduzi ya wananchi nchini humo.
Watunisia walijitokeza katika maeneo mbalimbali nchini humo katika Siku ya Quds na kutangaza mfungamano wao na wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina huku wakilaani vikali utawala wa Kizayuni wa Israel. Wakati wa dikteta aliyetimuliwa Zein al Abidine ben Ali, Watunisia hawakuwa na haki ya kuadhimisha siku ya Quds.
Akizungumza na kanali ya televisheni ya al Alam, Khalil Shahin mtaalamu wa masuala ya kisiasa wa Tunisia amesema, ‘Siku ya Quds ni tukio muhimu katika Ulimwengu wa Kiislamu ambapo mataifa yote hupata fursa ya kuwaunga mkono Wapalestina wanaodhulumiwa’.
Amesema njama za utawala bandia wa Israel za kuuyahudisha mji wa Quds na kufuta utambulisho wa Kiislamu na Kipalestina wa mji huo ni jambo ambapo linalowajibisha Waislamu wote duniani kuzingatia kadhia ya Quds.
849946
captcha