IQNA

Algeria yakanusha kuwa Gaddafi amekimbilia nchini humo

18:57 - August 28, 2011
Habari ID: 2178263
Wizara ya Mambo ya Nje ya Algeria imekanusha habari zinazodai kuwa dikteta wa Libya Kanali Muammar Gaddafi amekimbilia nchini humo akiwa pamoja na familia yake.
Serikali ya Algeria imetangaza kuwa hakuna uwezekano wowote kwamba Gaddafi na wanawe waliokuwa katika magari ya deraya wamekimbilia nchini Algeria.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Algeria amesema kuwa habari zinazodai kuwa gari iliyokuwa imembeba Gaddafi na familia yake imeingia nchini humo, hazina kweli wowote.
Vyama vya upinzani vya Libya pia vimetangaza kuwa hakuna taarifa yoyote kuhusu mahala alipo Muammar Gaddafi na wanawe. 851115


captcha