IQNA

Mwana wa Gadaffi, Saad akimbilia nchini Niger

12:21 - September 13, 2011
Habari ID: 2186116
Msemaji wa serikali ya Niger amesema kuwa Saad Gaddafi mwana wa dikteta wa Libya Muammar Gaddafi amevuka mpaka na kuingia katika ardhi ya nchi hiyo.
Marau Amadou Waziri wa Sheria wa Niger amesema kwamba, Saad aliingia Niger jana katika msafara wa watu 9. Ameongeza kwamba msafara huo ilikuwa ukielekea kusini katika eneo la Agadez ambako inaaminiwa kuwa maafisa wa ngazi za juu wa utawala wa Gaddafi wamejificha katika hoteli moja.
Niger pia imethibitisha kwamba majenerali watatu wa ngazi za juu wa utawala wa Gaddafi akiwemo Al Rifi Ali al Sharrif aliyekuwa mkuu wa kikosi cha anga cha Libya pia amewasili katika eneo la Agadez.
Mwana wa Gaddafi Saad mwenye umri wa miaka 37 ni shakhsia aliyekuwa na ushawishi mkubwa katika utawala ulioanguka wa Libya.
859260
captcha