Maombolezo ya kuhuisha kumbukumbu hiyo chungu yalifanyika katika miji mbalimbali ya Mashia nchini Saudia ikiwemo ya Qatif, Umm Hamam, Saihat na pia katika sehemu za mji wa Madina. Kikao muhimu cha maombolezo ya wanawake kilifanyika katika Kituo cha Hauraa mjini Hamam ambapo washiriki walikumbusha nafasi muhimu aliyokuwa nayo Imam Swadiq (as) katika kueneza mafundisho ya Uislamu halisi katika mazingira magumu ya maisha yake. Maombolezo mengine muhimu ya kukumbuka kifo cha Imam Swadiq (as) yalifanyika katika mji wa Qatif ambapo Sheikh Abdul Hayy Aal Qambar alihutubia waombolezaji. Maombolezo kama hayo yalifanyika katika Msikiti wa Imam Jawad (as) mjini Saihat ambapo Hujjatul Islam wal Muslimeen Ali Aal Suleis Yahya alizungumza. 866434