IQNA

Wazayuni wachoma moto msikiti wa kijiji cha al Khalil

17:50 - October 03, 2011
Habari ID: 2198247
Walowezi wa Kizayuni leo wamechoma moto msikiti wa kijiji cha Tuba ulioko katika eneo la al Khalil huko Palestina.
Gazet la al Intiqad linalochapishwa Lebanon limeandika kuwa Wazayuni wenye misimamo mikali wamechoma moto msikiti huo mepema leo na kuharibu sehemu yake kubwa.
Kabla ya kuchoma moto msikiti huo, walowezi hao wa Kizayuni waliandika nara za kibaguzi katika kuta za eneo hilo la ibada.
Ripoti zinasema kuwa baada ya kuchomwa moto msikiti huo kulitokea mapigano makali baina ya wakazi wa kijiji hicho na askari wa utawala ghasibu wa Israel.
Walowezi wa Kiyahudi wamezidisha mashambulizi na hujuma dhidi misikiti ya Waislamu huko Palestina. 872472

captcha