IQNA

Sherehe za kuzaliwa Imam Ridha (as) zafanyika Vienna

8:34 - October 10, 2011
Habari ID: 2201939
Sherehe za kuadhimisha siku ya kuzaliwa Imam Ridha (as) ambaye ni Imam wa Nane wa Waislamu wa madhehebu ya Shia na mmoja wa Watu wa Nyumba ya Mtume (as) zilifanyika Jumamosi iliyopita katika Kituo cha Kiislamu cha Imam Ridha (as) huko Vienna mji mkuu wa Austria.
Kwa mujibu wa Idara ya Mawasiliano ya Umma ya kituo hicho, sherehe hizo zilianza saa moja hadi saa tatu usiku.
Waislamu wanaoishi mjini humo walishiriki kwenye ratiba mbalimbali ambazo ziliandaliwa na kituo hicho kwa mnasaba huo wa furaha ambapo walielezea kufurahishwa kwao kwa kupata fursa za kushiriki kwenye shererehe hizo za kumuenzi na kumtukuza mtukufu huyo wa Ahlul Beit ya Mtume (saw). 875961
captcha