IQNA

Utawala wa Israel watoa amri ya kuharibiwa Msikiti wa Yafah

16:09 - October 10, 2011
Habari ID: 2202504
Utawala haramu wa Israel umetoa amri ya kubomolewa sehemu ya Msikiti wa Yafa ambao umedai uko kwenye ardhi zilizotekwa na utawala huo mwaka 1948.
Watawala wa utawala huo wametoa amri ya kubomelewa sehemu ya msikiti huo kwa kisingizio kuwa ulijengwa bila kibali cha serikali, katika hali ambayo ni siku chache tu zimepita tokea walowezi wa Kizayuni wavunjie heshima makaburi ya Waislamu na Wakristo katika mji huo.
Watawala hao wanasema wamechukua hatua ya kubomoa sehemu moja ya msikiti huo kutokana na kuwa iliongezwa kwenye msikiti mkuu bila ruhusa ya serikali.
Utawala haramu wa Israel umetoa muda wa miezi miwili kwa Waislamu wa mji huo wawe wamebomoa sehemu hiyo mpya la sivyo watawaamuru maafisa wa halmashauri ya mji huo kuibomoa. 876907
captcha