IQNA

Kwa kisingizio cha kuzuia fujo:

Saudia yazuia marasimu ya kujibari na washirikina

14:41 - October 16, 2011
Habari ID: 2205879
Viongozi wa Saudi Arabia wamepiga marufuku ibada ya kujibari na kujiweka mbali na washirikina inayofanywa na mahujaji wa Iran na maeneo mengine ya dunia katika Hija ya mwaka huu kwa kisingizio cha kuzuia fujo katika siku za ibada hiyo.
Saudi Arabia ilitangaza jana kwamba, kwa ajili ya kulinda amani na usalama wa mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu, hakuna ruhusa ya kufanya kitendo chochote kinachoweza kuzusha fujo katika siku za ibada ya hija ya mwaka huu!
Amir wa eneo la Makka Khalid Faisal amewaambia waandishi habari kwamba serikali haitaruhusu mtu yeyote kufanya tendo litakalohatarisha amani ya mahujaji.
Amir wa Makka amesema kuwa hadi sasa zaidi ya mahujai nusu milioni wamekwishawasili nchini Saudi Arabia na kwamba juhudi zinafanyika kwa shabaha ya kuboresha huduma kwa mahujaji hao. 880725
captcha