IQNA

Kiongozi wa Jamaat Islamiya Pakistan:

Mustakbali ni wa Uislamu

17:05 - October 17, 2011
Habari ID: 2206678
Kiongozi wa kundi la Jamaat Islamiya la Pakistan amesema kuwa mustakbali ni wa dini ya Kiislamu kwani dini hiyo ndiyo mfumo pekee unaoweza kutatua matatizo yote ya kijamii na kuleta amani na usalama kote duniani.
Munawwar Hassan amesema katika hotuba aliyotoa kwenye Chuo Kikuu cha Punjab katika mji wa Lahore kwamba maandamano yanayofanywa na maelfu ya watu barani Ulaya na Marekani yameonyesha kwamba hawana tena imani na mfumo wa ubepari.
Amesema kuwa huko nyuma tulishuhudia kushindwa mifumo ya kikomunisti na kisoshalisti na sasa wananchi wa huko Magharibi wanatangaza kutokuwa na imani tena na mfumo wa kibepari.
Kiongozi wa kundi la Jamaat Islamiya la Pakistan amesema kuwa mfumo wa Kiislamu ndio unaoweza kumuondoa mwanadamu katika minyororo ya kuwa mtumwa wa mwanadamu mwenzake na kumuelekeza kwa Mwenyezi Mungu. 881412

captcha