IQNA

Wanamapinduzi wa Libya wagundua maficho ya Gaddafi

22:04 - October 18, 2011
Habari ID: 2207550
Kamanda mmoja wa kitengo cha upelelezi cha Baraza la Taifa la Mpito la Libya katika eneo la Bu Hadi katika mji wa Sirte amesema kuwa kikosi chake kimegundua mahala alipojificha dikteta mtoro wa nchi hiyo Muammar Gaddafi na kwamba dikteta huyo atatiwa nguvuni siku chache zijazo.
Salim Miftah al Rafadi amesisitiza kuwa kikosi chake kimegundua maficho ya dikteta Gaddafi katika mji alikozaliwa wa Sirte. Amesema dikteta huyo atatiwa nguvuni hivi karibuni na kwamba kubakia kwake huru ni hatari kubwa kwa amani na usalama wa Libya.
Awali makamanda wa Baraza la Taifa la Mpito la Libya walikuwa wametangaza kuwa Gaddafi amejifisha katika eneo la jangwani la kusini magharibi mwa Libya karibu na mji wa Gaddamis.
Kamanda al Rafadi amesema wanamapinduzi wa Libya wanauzingira mji wa Sirte kutokea pande zote na kwamba hakuna uwezekano wa Muammar Gaddafi kutoroka mji huo. 882531


captcha