Gazeti la al Watan la Saudi Arabia limeripoti kuwa Saadi Gaddafi aliwasili nchini humo akifuatana na kiongozi mmoja wa ngazi za juu wa Saudia.
Gazeti hilo limeripoti kuwa Saadi alipelekwa Saudia na ndege ya Uturuki na kwamba safari hiyo imetayarishwa na Mawahabi wa nchi hiyo.
Ni vyema kukumbusha kuwa Saadi Gaddafi alikimbilia Niger baada ya mji wa Tripoli kutekwa na wanamapinduzi wa Libya na kusambaratika serikali ya baba yake, Muammar Gaddafi. 890052