IQNA

Filamu ya 'Waislamu wote wa Marekani' kuonyeshwa

17:27 - November 02, 2011
Habari ID: 2216529
Sehemu ya kwanza ya filamu ya televisheni ya 'Waislamu wote wa Marekani' imepangwa kuanza kuonyeshwa tarehe 13 Novemba ikiwa ni katika juhudi za kuarifisha maisha halisi ya Waislamu nchini humo.
Kwa mujibu wa tovuti ya saphirnews, sehemu ya kwanza ya filamu hiyo ambayo imegawanywa katika sehemu 8, na ambayo ina lengo la kuarifisha mila na desturi za Waislamu na kuondoa dhana mbaya iliyoko katika jamii ya Wamarekani kuhusiana na Uislamu, itaanza kuonyeshwa tarehe iliyotajwa kupitia televisheni ya TLC.
Filamu hiyo inazungumzia maisha ya kawaida ya familia tano za Kiislamu zikiwa nyumbani kwao na kwenye misikiti. Familia hizo zinaishi katika viunga vya mji wa Detroit katika jimbo la Michigan Marekani.
Waongozaji wa filamu hiyo hawakuuchagua mji huo kisadfa tu bila dalili yoyote, bali ni kutokana na ukweli kuwa mji huo ndio ulio na msikiti mkubwa zaidi kaskazini mwa Marekani. Sababu nyingine ni kuwa Waislamu wamekuwa wakiishi katika mji huo kwa miaka mingi. 891881
captcha