Gazeti la al Ahram limeripoti kuwa Ali Abdul Fattah amesema harakati hiyo haitatupilia mbali kaulimbiu hiyo katika kampeni za uchaguzi ujao. Amesema kaulimbiu hiyo ni nara ya kisheria inayobainisha itikadi za Ikhwanul Muslimin na si nara ya kidini pekee.
Amesisitiza kuwa wagombea wengine wa kujitegemea pia wanatumia nara hiyo.
Uchaguzi wa bunge la Misri utafanyika tarehe 27 Novemba. 895553