IQNA

Kikao cha Kimataifa cha Imam Muhammad Ghazali

13:40 - November 13, 2011
Habari ID: 2221715
Kikao cha Kimataifa chenye anwani ya "Muhammad Ghazali; Miaka 900 baada ya Kifo cha Mwislamu Mwanafikra Mkubwa wa Dunia" kitafanyika Ijumaa Disemba Pili mjini Paris, Ufaransa.
Kwa mujibu wa Sphirnews, programu hiyo imeandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiislamu (Institut des Hautes Etudes Islamiques) kwa ushirikiano na Shirika la Kiislamu la Elimu, Utamaduni na Sayansi (ISESCO) pamoja na Idara ya Masomo ya Mashariki katika Chuo Kikuu cha Strasbourg.
Sherehe ya ufunguzi itahutubiwa na Mona Khazindar Mkuu wa Taasisi ya Ulimwengu wa Kiarabu mjini Paris, Bariza Khiari Naibu Spika wa Baraza la Senate Ufaransa na Dr. Abdulazizi Othman Altwaijri Mkurugenzi Mkuu wa ISESCO.
897059
captcha