IQNA

Vyombo vya habari vya Kiislamu duniani vyatakiwa kushirikiana

22:23 - November 27, 2011
Habari ID: 2229989
Vyombo vya habari vya Kiislamu duniani vimetakiwa kuimarisha ushirikiano ili kubadilishana uzoefu na kwa njia hiyo kuhakikisha kuwa kunakuwepo mshikamano na umoja baina yao.
Hayo yamesemwa na Hujjatul Islam Sayyid Ali Taheri Mbunge na mwanachama wa Tume ya Utamaduni katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran.
Amesema vyombo vya habari vya Kiislamu vilifanikiwa kueneza habari za mwamko wa Kiislamu na hivyo kuangusha ubeberu wa vyombo vya habari vya kimagharibi.
Hujjatul Islam Taheri ameashiria kampeni chafu za vyombo vya habari vya Magharibi dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na kusema kampeni hiyo imefeli kutokana na kuenea vyombo vya habari vya Kiislamu duniani.
905598
captcha