Mahafidhi hao walishiriki katika shughuli za maombolezo katika msafara ulioanzia kwenye Haram ya Abul Fadhl Abbas hadi kwenye Haram ya Imam Hussein (as).
Katika kipindi chote cha maombolezo hayo mahafidhi hao walikariri nara kuhusu harakati ya mapambano ya Imam Hussein (as) na mafundisho ya Qur'ani Tukufu huku wakiwa wamebeba nakala za kitabu hicho na bendera zenye rangi nyeusi.
Mahudhurio makubwa ya makari na mahafidhi wa Qur'ani Tukufu wa Darul Qur'an katika maombolezo ya siku ya Ashura yamefanyika kwa mpangilio maalumu na kuwavutia watu wengi waliokwenda kwenye Haram ya Imam Hussein kwa ajili ya ziara.
Kundi hilo la mahafidhi wa Qur'ani Tukufu la Haram ya Imam Hussein (as) lilianzishwa miaka mitatu iliyopita kwa shabaha ya kuwahamasisha makari wa Qur'ani kushiriki kwa wingi katika marasimu na maombolezo ya kukumbuka tukio la kuuawa Bwana wa Mashahidi Imam Hussein bin Ali (as). 911801