IQNA

Ikhwanul Muslimin wazidi kupata ushindi katika uchaguzi Misri

23:55 - December 07, 2011
Habari ID: 2235034
Kundi la Ikhwanul Muslimin nchini Misri limezidi kupata ushindi katika uchaguzi wa Bunge wa nchi hiyo baada ya kupata wingi mutlaki wa viti 35 kati ya viti 56 vilivyogombaniwa katika awamu ya pili ya uchaguzi huo.
Tume ya Uchaguzi ya Misri leo jioni imetangaza matokeo ya mwisho ya awamu ya pili ya uchaguzi wa Bunge nchini humo, uliofanyika kwenye mikoa 9 na kusema kuwa, Chama cha Uhuru na Uadilifu ambacho ni tawi la kisiasa la kundi la Ikhwanul Muslimin kimefanikiwa kupata ushindi mkubwa wa asilimia 62 ya viti vilivyowaniwa.
Vyama vingine vilivyoshiriki kwenye awamu hii ya pili ya uchaguzi huo ni kile cha kisalafi cha an Nur kilichopata viti 5, na wagombea binafsi ambao wamepata viti 7.
Kundi la Ikhwanul Muslimin lilipata ushindi mkubwa pia katika awamu ya kwanza ya uchaguzi huo wa kihistoria.
Awamu nyingine za uchaguzi huo zitafanyika katika siku za usoni na tayari imetabiriwa kuwa, wanaharakati wa Kiislamu wataendelea kupata ushindi katika awamu hizo pia.
911423
captcha