Warsha hiyo itawakutanisha pamoja wakuu 20 wa shule za Kiislamu-Kiarabu kutoka Algeria, Tunisia, Senegal, Guinea, Guinea Bissau, Burkina Faso, Morocco, Mauritania na Mali.
Warsha hiyo inalenga kuimarisha shule za Kiislamu Kiarabu kwa kuangazia matatizo ya kiakademiki, kielimu, kifedha na mfumo wa usimamizi.
Washiriki pia watachunguza njia za kivitendo za kuimarisha kiwango cha elimu katika shule hizo pamoja na kuzijumuisha na shule za kawaida zisizo za kidini.
Vilevile washiriki watabadilishana mawazo na uzoefu kuhusu shule za Kiislamu-Kiarabu na kuangazia mustakabali wa shule hizo.
Youssef Abou Daka wa ISESCO ambaye ni mtaalamu wa masuala ya elimu atasimamia warsha hiyo.
920276