IQNA

OIC yaonya juu ya hali mbaya ya afya katika Ukanda wa Gaza

16:00 - January 04, 2012
Habari ID: 2251060
Ekmeleddin Ihsanoglu, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) ametoa taarifa akitaka misaada ya dharura ya kitiba ifikishwe kwa wakazi wa Ukanda wa Gaza kwa ajili ya kukabiliana na hali mbaya ya afya inayoukabili ukanda huo.
Huku akibainisha mgogoro mkubwa wa kiafya unaowakabili wagonjwa wa saratani na uhaba wa suhula za kuwatibu watu wenye matatizo ya figo, Ihsanoglu ameziomba nchi wanachama wa OIC pamoja na mashirika ya misaada ya kibinadamu kufanya juhudi za kuwasaidia wakazi wa Ukanda wa Gaza.
Ofisi za OIC mjini Gaza na Cairo zimetangaza kuwa ziko tayari kufanya utaratibu wa kutumwa misaada hiyo katika ukanda huo.
Uhaba wa suhula za tiba na madawa ya magonjwa sugu unahatarisha maisha ya wagonjwa wengi wa ukanda huo na hata upasuaji wa magonjwa ya macho, watoto na moyo umesimama kabisa. 928744
captcha