Kwa mujibu wa gazeti la Le Figaro la Ufaransa Ki-Moon alitoa tahadhari ya kusimamishwa ujenzi wa vitongoji hivyo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari huko Beirut mji mkuu wa Lebanon. Amesema ujenzi wa vitongoji hivyo unapasa kusimama mara moja kwa sababu unazuia kuundwa kwa nchi huru ya Palestina.
Katika sehemu nyingine ya matamshi yake, Ban Ki-moon amesema kuwa vitongoji vyote vya zamani na vya sasa ni haramu na kwamba vinapaswa kusimamishwa.
Vilevile amelaani vitendo vya mabavu na mashambulio yanayofanywa na askari wa utawala haramu wa Israel dhidi ya raia wasio na hatia wa Palestina na kusisitiza kuwa jambo hilo haliwezi kuvumiliwa wala kukubalika. Amesema tayari Umoja wa Mataifa umewaonya watawala wa Tel Aviv kuhusiana suala hilo. 936011