Kwa mujibu wa The Sunday Canberra Times, Shirikisho la Mabaraza ya Kiislamu Australia limesema katika ombi lake hilo kuwa: 'Mchango wa Waislamu katika ustawi wa Australia ni sehemu ya turathi ya Waustralia wote, kwa hivyo tunaomba kupewa kipande cha ardhi mjini Canberra'.
Waislamu waliwasilisha ombi lao hilo Aprili 2011 na wanakusudia kujenga 'Jengo la Makumbusho la Historia na Sanaa ya Kiislamu'.
Akiwasilisha ombi hilo, Mwenyekiti wa Shirikisho la Mabaraza ya Kiislamu Australia amesema jengo hilo la makumbusho litakuwa na mchango mkubwa katika mji wa Canberra na litawaelimisha Waustralia kuhusu turathi ya Waislamu huko Australia katika kipindi cha karne mbili zilizopita.
935860