IQNA

Maisha ya hafidhi wa Qur'ani wa Pakistan kuchunguza Bahrain

17:30 - January 23, 2012
Habari ID: 2261549
Sira na maisha ya hafidhi asiyeona wa Qur'ani Tukufu wa Pakistan yatachunguzwa katika kongamano litakalofanyika kwa ushirikiano wa ubalozi wa Pakistan nchini Bahrain chini ya usimamizi wa Kituo cha Utafiti wa Masuala ya Kiutamaduni na Elimu za Kiislamu Marekani na Canada.
Kongamano hilo litachunguza sira na maisha ya Prf. Muhammad Abdullah Qadari, hafidhi kipofu wa Pakistan kama msomi anayefanya bidii kubwa wa Qur'ani.
Prf. Qadari ambaye alizaliwa akiwa kipofu aliweza kuhifadhi Qur'ani nzima kwa kufanya juhudi kubwa na kupata shahada ya uzamivu katika taaluma ya siasa.
Mbali na Qur'ani Tukufu Muhammad Qadari amehifadhi vitabu 200 vikiwemo vya Plato, Aristotle, vitabu vya lugha ya Kiarabu na kadhalika.
Vilevile anazungumza lugha kadhaa zikiwemo za Kiarabu, Kiingereza na Kifarsi. 939660
captcha