IQNA

Mafunzo ya muda ya Qur’ani kutolewa Marekani

18:44 - January 25, 2012
Habari ID: 2262374
Mafunzo ya muda ya Siri za Qur’ani yatatolewa kwa kipindi cha wiki 12 katika Chuo Kikuu cha Irfan na Tiba ya Kiroho (USHS) katika mji wa Angwin nchini Marekani.
Kwa mujibu wa tovuti ya Sufiuniversity, mafunzo hayo yataanza tarehe 15 Februari hadi Mei 3.
Miongoni mwa masuala yatakayojadiliwa katika mafunzo hayo ni pamoja na Qur’an Tukufu, risara ya
upendo ya Mwenyezi Mungu, utambuzi wa aya zinazotoa tiba za Qur’ani, njia za kutumia Qur’ani
Tukufu, maarifa ya kina ya Qur’ani, utakatifu wa Qur’ani, chakula cha kiroho cha Qur’ani na kadhalika.
Baada ya kukamilisha mafunzo hayo, wahitimu wanaweza kushiriki katika duru ya pili ya mafunzo ya siri za Qur’ani Tukufu katika chuo hicho. 940723
captcha