IQNA

Masomo ya tajwidi ya Qur'ani kufanyika Doha

12:16 - February 02, 2012
Habari ID: 2266952
Masomo ya muda mfupi ya tajwidi ya Qur'ani Tukufu yamepangwa kufanyika hivi karibuni katika Msikiti wa Hamad bin Khalid mjini Doha Qatar ambapo mahafidh mashuhuri wa Qur'ani kutoka kila pembe za nchi hiyo wanatazamiwa kushiriki.
Sayyid Hamad bin Abdallah al-Mihna, Naibu Mkuu wa Idara ya Tablighi na Mwongozo wa Kidini inayofungamana na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Qatar amesema kwamba kuimarishwa uwezo wa mahafidh wa Qur'ani katika vituo vya Qur'ani vya Qatar na vilevile kunyanyuliwa kiwango cha usomaji sahihi wa kitabu hicho kitakatifu cha mbinguni ni miongoni mwa malengo ya kuandaliwa masomo hayo.
Amesema licha ya kuwa watu wanaoshiriki katika masomo hayo kimsingi ni walimu na mahafidh wa Qura'ni, lakini walimu wa masomo mengine ya Kiislamu na vilevile wanachuo wa Qatar wanaweza pia kushiriki.
Masomo hayo yamepangwa kufanyika kwa muda wa siku kumi kati ya swala mbili za Maghrib na Ishaa. Kwa mujibu wa ripoti hiyo zaidi ya mahafidh na walimu wa Qur'ani 100 wamejiandikisha kushiriki masomo hayo. 945164
captcha