Qur'ani hii ilitarjumiwa mwaka 1787 kwa amri ya Malkia Ekaterina II kwa mujibu wa tarjumi ya wanazuoni wa Tatarstan.
Nuskha hii baadaye ilitumiwa kama kigezo cha misahafu yote ya lugha ya Kirusi ambayo inatumiwa na Waislamu wa Russia.
Kuna Qur'ani 600 zilizotarjumiwa kwa lugha mbalimbali katika Jumba la Makumbusho la Kiislamu katika eneo la Kazan Kremlin nchini Russia.
'Mwaka wa Qur'ani Tatarstan utawawezesha wakazi wa eneo hilo kufahamu mafundisho ya Qur'ani, amesema Ildus Xazra Faizvo Mufti wa Tatarstan.
Jamhuri ya Tatarstan ambayo mji wake mkuu ni Kazan ni sehemu ya Shirikisho la Russia na iko katika Jimbo la Volga.
947495