Tovuti ya Turkia al Youm imeripoti kuwa Mulla Abdullah Farly alikuwa mtu wa kwanza aliyetarjumu tafsiri ya Qur'ani Tukufu kwa lugha ya Kikurdi hapo mwaka 1997.
Mulla Abdullah Farly alikuwa miongoni mwa wanaharakati wa masuala ya Qur'ani wa Uturuki na alifanya uhakiki mkubwa kuhusu mshairi na mwanafasihi mashuhuri wa Kikurdi Ahmad Khani.
Mwili wa mwanaharakati huyo wa masuala ya Qur'ani ulizikwa jana katika mji alikozaliwa wa Van huko mashariki mwa Uturuki. 947603