IQNA

Kikao cha Sira ya Mtume SAW chafanyika Tanzania

15:59 - February 13, 2012
Habari ID: 2273358
Kikao cha Sira ya Mtume SAW kimefanyika kwa mnasaba wa Milad-un-Nabii na wilada ya Imam Ja'afar Sadiq AS huko Dar-es-Salaam, Tanzania.
Kikao hicho kiliandaliwa na Chuo cha Kiislamu cha Imam Sadiq AS mjini Dar-es-Salaam na kuhudhuriwa na idadi kubwa ya Waislamu nchini Tanzania.
Kikao hicho kilianza kwa kisomo cha Qur'ani Tukufu na kufuatiwa na qasida zilizotayarishwa na wanafunzi wa chuo hicho cha kidini.
Hafla hiyo ilifanyika kuanzia tarehe 17 Rabi'ul Awwal na kuhutubiwa na mkuu wa chuo hicho Sheikh Hemed Jalala ambaye alizungumzia shakhsia ya Mtume SAW na Imam Ja'afar Sadiq AS.
Hafla hiyo ya Maulidi ni kati ya sherehe ambazo hufanywa na Waislamu wa Tanzania. Sherehe za Maulidi nchini Tanzania sawa na maeneo mengine ya Afrika Mashariki huanza 12 Rabi'ul Awwal na kuendelea kwa miezi miwili katika miji mbalimbali ya eneo hilo.
951820
captcha