IQNA

Baada ya kushadidi malalamiko ya Waislamu wanaopinga kuvunjiwa heshima Qur'ani:

Ubalozi wa Marekani Afghanistan wafungwa

17:35 - February 22, 2012
Habari ID: 2279138
Ubalozi wa Marekani mjini Kabul, Afghanistan umefungwa leo siku mbili tu baada ya askari wa nchi hiyo kuvunjia heshima kitabu kitakatifu cha Qur'ani.
Tovuti ya Bloomberg imeripoti kuwa maandamano na mikusanyiko ya maelfu ya wananchi wenye hasira wa Afghanistan dhidi ya kitendo cha askari wa Marekani cha kuchoma moto Qur'ani Tukufu yamewalazimisha maafisa wa Marekani kufunga ubalozi wao mjini Kabul.
Ubalozi wa Marekani Afghanistan umetangaza kuwa ofisi zake zimefungwa hadi hapo baadaye na umewataka wafanyakazi wake wote kufika ubalozini hapo haraka iwezekanavyo.
Maafisa wa Marekani nchini Afghanistan pia wamewapiga marufuku wafanyakazi wa Kimarekani kufanya safari katika mji wa Qandahar ambao ni wa pili kwa ukubwa nchini Afghanistan.
Askari wa Marekani katika kambi ya jeshi la anga ya Bagram jana walichoma moto vitabu vya Kiislamu zikiwemo nakama za kitabu kitakatifu cha Qur'ani. 958640



captcha