Wanazuoni hao 41 wa mkoa wa Ahsaa wamesema ukandamizaji huo hauwezi kuvumiliwa na wamewataka watawala wa Riyadh kuanzisha mara moja uchunguzi wa kina kuhusiana na mauaji ya vijana wa Kishia nchini humo.
Sehemu moja ya taarifa hiyo imewataka watawala wa Saudia kuondoa vituo vya upekuzi vilivyowekwa katika maeneo ya kuingia katika miji ya Mashia na pia kuondoa marufuku ya ujenzi wa misikiti na huseinia za Mashia pamoja na kuheshimu matukufu yao. Wamesema kuendelea kwa ukandamizaji na uonevu huo wa watawala wa Saudia dhidi ya Mashia kutazidisha tu mgogoro wa nchi hiyo.
Mambo mengine yanayofuatiliwa na wanazuoni hao wa Kishia ni kuondolewa marufuku ya kuchapishwa vitabu vya Mashia na pia kufuta matusi na uvunjiwaji heshima itikadi za Kishia katika vitabu vya masomo nchini humo. Wamesisitiza kwamba kupuuzwa kwa matakwa hayo na kuendelea kukandamizwa Mashia kutazidisha mgogoro wa nchi hiyo. 959268