IQNA

Mashindano ya Qur'ani yamalizika Riyadh

17:03 - March 04, 2012
Habari ID: 2285403
Duru ya 14 ya mashindano ya Qur'ani Tukufu yamekamilika leo Jumapili huko Riyadh mji mkuu wa Saudi Arabia.
Kwa mujibu wa gazeti la Arab News, mashindano hayo ambayo yameandaliwa na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Saudia kwa usimamizi wa Salman bin Abdul Aziz, Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo yalianza tarehe 27 Februari. Mashindano hayo yameendelea kwa kushirikishwa washindani 51 wa kiume na 40 wa kike. Washindi wa mwisho watatangazwa baadaye leo na kutunukiwa zawadi nono. Mashindano hayo huandaliwa kila mwaka na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu kwa madhumuni ya kueneza na kutekelezwa mafundisho ya Qur'ani Tukufu katika maisha ya mwanadamu. 964494
captcha