IQNA

Mafunzo ya Qur'ani kuwa ya lazima katika jimbo la Punjab nchini Pakistan

13:53 - March 10, 2012
Habari ID: 2288853
Bunge la Jimbo la Punjab limepitisha mswada ambao utafanya mafunzo ya Qur'ani Tukufu katika shule zote za jimbo hilo kuwa ya lazima kuanzia mwakani.
Jimbo hilo ni moja ya majimbo manne ambayo yamepitisha mswaada wa kufanya mafunzo hayo kuwa ya lazima. Viongozi wa majimbo hayo wana matumaini kwamba jambo hilo litasaidia kueneza mafundisho ya dini ya Kiislamu miongoni mwa wakazi wake. Kabla ya hapo ni juzuu chache tu za Qur'ani ndizo zimekuwa zikifundishwa katika shule hizo lakini kutokea sasa kitabu hicho kizima pamoja na tafsiri ya aya zake itakuwa ikifundishwa katika shule hizo. 968297
captcha