IQNA

Mashindano ya 22 ya Qur'ani yaanza Oman

17:03 - March 14, 2012
Habari ID: 2291965
Duru ya mwanzo ya mashindano ya 22 ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani Tukufu itaanza Jumamosi ijayo mjini Muscat, Oman.
Gazeti la Oman News limeripoti kuwa, watu wanaotaka kushiriki mashindano hayo walikuwa na fursa ya kujiandikisha hadi leo Jumatano.
Mashindano hayo yatafanyika katika nyanja tano za hifdhi na tajwidi ya Qur'ani nzima, hifdhi na tajwidi ya juzuu 24, hifdhi na tajwidi ya juzuu 18, hifdhi na tajwidi ya juzuu 12, na hifdhi na tajwidi ya juzuu 12.
Washindi wa duru hii ya mashindano ya Qur'ani watachuana tena katika duru ya mwisho itakayofanyika hapo baadaye.
Duru ya 21 ya mashindano ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani Tukufu ya Oman ilifanyika mwaka jana ikiwashirikisha washindani 614. 971912
captcha