IQNA

Mafunzo ya muda ya Qur'ani kwa wasioona Chechnia

18:14 - April 09, 2012
Habari ID: 2301227
Mafunzo ya muda ya Qur'ani Tukufu makhsusi kwa ajili ya walemavu wa macho yalianza kutolewa jana katika Chuo cha Kiislamu cha Arsanov katika mji mkuu wa Chechnia, Grozny.
Mwalimu wa lugha ya Kiarabu wa chuo hicho Ramadhan Mustafaov amesema kuwa mafunzo hayo ya Qur'ani na lugha ya Kiarabu yanahudhuriwa na walemavu wa macho kutoka jamhuri za Ingushetia, Dagestan, Chechnia na Russia.
Ameongeza kuwa Chuo cha Arsanov ndicho kilichobunu fikra ya kuanzisha mafunzo hayo na ndicho kinachoyagharimia.
Ramadhan Mustafanov amesema kuwa kwa kutilia maanani kwamba mafunzo hayo yamewavutia watu wengi wenye ulemavu wa macho, chuo cha Kiislamu cha Arsanov kimeamua kutoa masomo hayo muda wote wa mwaka mzima. 981870
captcha