Mwakilishi wa IQNA kanda ya Afrika amesema kuwa semina hiyo itafanyika tarehe 13 Aprili saa tatu asubuhi na kuendela hadi kabla ya Sala ya Ijumaa. Amesema semina hiyo itahutubiwa na maulamaa kadhaa akiwemo mwanazuoni mashuhuri Sayyid Aidarus.
Kabla ya kuanza semina hiyo Karii bora wa kisiwa cha Lamu Abdul Ghani Othman al Khatib atasoma aya za Qur’ani na baada ya hapo mahatibu na maulama wa kidini watatoa hotuba wakizungumzia sira na mwenendo wa kiakhlaki wa Ahlul Bait (as). 983410