IQNA

Mpango wa Mafundisho ya Qur'ani Algeria

13:54 - May 08, 2012
Habari ID: 2321288
Taasisi ya Kimataifa ya Abul Hudaa ya Algeria imeanzisha rasmi mpango wa kitaifa wa harakati za Qur'ani utakaohusu mafundisho na masomo ya tajwidi kote katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
Kwa mujibu wa tovuti ya echoruoukonline, taasisi ya Abul Hudaa imezindua mpango huo katika mjii mkuu Algiers.
Mpango huo pia unajumuisha maonyesho kuhusu aina 10 za qiraa ya Qu'ani Tukufu, qiraa bora za Qur'ani Tukufu na vilevile vikao maalumu kuhusu ufahamu wa tajwidi katika miji mbalimbali ya Algeria.
Mpango huo pia utakuwa na darsa za Qur'ani na historia ya Qur'ani.
Waandalizi wa mpango huo wamesema watatumia teknolojia za kisasa katika kutoa mafundisho ya tajwidi.
Pembizoni mwa mafundisho hayo kutakuwa na mpango wa mashindano ya qiraa miongoni mwa familia ili kutathmini ujuzi waliopata washiriki.
1002984
captcha