IQNA

Mwanaharakati wa Qur'ani:

Wanigeria bado wanatumia mbinu za zamani za kufunza Qur'ani

17:51 - May 09, 2012
Habari ID: 2322442
Nigeria hado iko nyuma katika masuala ya teknolojia ya kisasa na kwa msingi huo wanafunzi wa Qur'ani wangali wanatumia mbinu na suhula za zamani za kufundishia Qur'ani.
Hayo yamesemwa na mwanaharakati wa Kiislamu wa Nigeria Ibrahim Mussa, katika mahojiano yake ya IQNA. Amesema kwa kawaida mafundisho ya Qur'ani huanza katika kipindi cha umri wa miaka minne wakati mtoto anapoanza kuzungumza na kuelewa anayoambiwa na mwanzoni hufunzwa sura fupi fupi za Qur'ani Tukufu.
Ibrahim Mussa ameongeza kuwa katika maeneo ya kaskazini mwa Nigeria watoto wadogo hupelekwa kwa mwalimu wa Qur'ani baada ya kuhifadhi Qur'ani. Mussa ambaye ni mhariri wa gazeti la al Mizan anasema mbali na madrasa za kijadi, Qur'ani pia hufundishwa katika shule za Kiislamu.
Amesema kuwa katika shule hizo za Qur'ani hutayarishwa mashindano makali ambayo yanazidisha hamu za kujifunza na kupata elimu na mafundisho zaidi ya Qur'ani baina ya wanafunzi.
Amesema kuwa makarii wa Qur'ani nchini Nigeria hufuatilia kiraa ya wasomaji mashuhuri duniani kama Minshawi na wengineo na mara nyingi hutumia kaseti na sidi za sauti za makarii hao. 1002009


captcha