IQNA

Mawahabi watishia kushambulia Haram ya Bibi Rukia (as) mjini Damascus

18:00 - May 21, 2012
Habari ID: 2330989
Afisa mmoja wa ngazi za juu nchini Syria amefichua habari za vitisho vya Mawahabi za kutaka kushambulia Haram ya Bibi Rukia (as) mjini Damascus.
Kwa mujibu wa tovuti ya Nun afisa huyo amesema kuwa ujumbe huo ulitumwa kwa idara inayosimamia eneo hilo takatifu la ziara na makundi ya magaidi wa Kiwahabi. Afisa huyo amesema kuwa ujumbe huo wa kushambuliwa Haram ya Bibi Rukia umetumwa kwa idara hiyo sambamba na kuongezeka mashambulio ya kigaidi ya Mawahabi dhidi ya Mashia mjini Damascus. Katika shambulio lao la hivi karibuni dhidi ya Mashia, Mawahabi wameshambulia na kumuua shahidi imamu wa Msikiti wa Bibi Rukia (as). Kwa mujibu wa ripoti hiyo hatua kali za kiusalama zimechukuliwa kwa ajili ya kuilinda Haram ya Bibi Rukia kutokana na mashambulio ya magaidi wa Kiwahabi. Kabla ya hapo magaidi hao walishambulia kwa risasi na kumuua shahidi Sayyid Nasir al-Alawi, hatibu na imamu wa swala ya jamaa wa Husseiniya ya Alawiya katika eneo la Zeinabiya katika mji wa Damascus. 1012115
captcha