Katika mlipuko wa bomu huko Baghdad siku ya Jumatatu karibu watu 32 waliuawa .
Mlipuko huo ulitokea karibu na ofisi za iadara ya Waqfu wa Mashia katika eneo la Babul Muadham lililoko mjini Baghdad ambapo wengine wapatao 100 walijeruhiwa. Katika tukio hilo la kigaidi nyumba kadhaa za idara hiyo pia zimeharibiwa huku wafanyakazi wengi wa idara hiyo wakiwemo polisi wa usalama wakiuawa. Kufuatia tukio hilo vikosi vya usalama vya mjini Baghdad vimezingira eneo la tukio hilo na kuanzisha uchunguzi ili kuwatia nguvuni waliohusika na tukio hilo la kigaidi.
Viongozi wa Kishia na Kisunni Iraq katika taarifa yao wametoa wito kwa Waislamu wa madhehebu yote Iraq kudumisha utulivu na kuwatahadharisha wasitumbukie katika mtego wa maadui.
Spika wa Bunge la Iraq Osama Al Najifi ambaye ni Msunni amewataka Wairaqi waungane kukabiliana na maadui wa taifa hilo.
1023012