IQNA

Hijabu yapigwa marufuku Brussels

18:04 - June 05, 2012
Habari ID: 2340615
Wakuu wa shule za msingi na sekondari 94 mjini Brussels mji mkuu wa Ubelgiji wamepiga marufuku vazi la hijabu ambalo ni vazi la stara na heshima kwa mwanamke wa Kiislamu.
Kuna shule 98 kama hizo mjini humo lakini ni nne tu kati ya hizo ndizo zinawaruhusu wanafunzi wa kike kuhudhuria masomo yao wakiwa wamevalia vazi hilo la heshima. Inasemekana kuwa shule mbili kati ya hizo pia kuanzia mwaka huu wa masomo zimekuwa zikiwazuia mabinti wa Kiislamu kuhudhuria masomo yao wakiwa wamevalia hijabu na hivyo kufanya idadi ya shule zinazowazuia wanafunzi kuhudhuria masomo wakiwa wamevalia vazi hilo la stara kwa mwanamke wa Kiislamu kufikia 96. Maeneo tofauti ya Ubelgiji hutekeleza sheria tofauti kuhusiana na mavazi yanayopasa kuvaliwa na wanafunzi. Kwa mfano tokea mwaka 2009 shule 700 za jimbo la Flanders zimepiga marufuku hijabu kwa wanafunzi wa shule hizo. 1023233
captcha