IQNA

Ikhwan ya Jordan yasisitiza uungaji mkono kwa Wapalestina

18:55 - June 11, 2012
Habari ID: 2344550
Akizungumza na wananchi wa Palestina mara tu baada ya kuwasili huko katika Ukanda wa Gaza, kiongozi wa kundi la Ikhwanul Muslimin la nchini Jordan amesisitiza kwamba Wapalestina hao hawako peke yao katika jitihada zao za kupambana na dhulma ya utawala haramu wa Israel.
Kwa mujibu wa tovuti ya guysen, Said Hamam ambaye ni kiongozi wa Ikhwanul Muslimin ya Jordan ameongoza ujumbe wa zaidi ya wanaharakati 100 wa Kiislamu wa nchi hiyo katika safari yake hiyo katika Ukanda wa Gaza. Ujumbe huo umewapelekea misaada ya madawa wakazi wa ukanda huo ambao wanakabiliwa na matatizo mengi kutokana na mzingiro wa kidhulma unaotekelezwa dhidi yao na utawala haramu wa Israel. Ujumbe huo umetoa taarifa ukimuhutubu Ismail Hania Waziri Mkuu wa serikali ya Palestina kwa kusema kwamba wasikate tamaa na kudhani kwamba wako peke yao katika mapambano yao dhidi ya dhulma ya utawala haramu wa Israel na kutaka kuvunja mzingiro uliotajwa, bali ndugu zao wa Jordan wako pamoja nao katika mapambano yao hayo. 1027334
captcha