Ripota wa IQNA amesema kuwa kongamano hilo la kidini lilihudhuriwa na wanafunzi wa vyuo vikuu na kuhutubiwa na mwandishi na mhakiki wa sayansi za Kiislamu nchini Uturuki Muhammad Amin Yildirim.
Msomi huyo ambaye amefanya uhakiki kwa miaka mingi kuhusu sayansi na elimu za Kiislamu amesisitiza juu ya udharura wa kutegemewa sira na maagizo ya Mtume Muhammad (saw) katika masuala yote ya maisha.
Mwandishi huyo wa Kiislamu wa Uturuki ameashiria kipindi cha mwanzoni mwa Uislamu na maisha ya zama hizo na kufanya ulinganisho wa kipindi hicho na zama za sasa. 1031123