IQNA

Mashia wa Saudi Arabia walalamikia kutiwa mbaraoni Ayatullah Namr

12:52 - July 09, 2012
Habari ID: 2364203
Waislamu wa madhehebu ya Shia wakazi wa mji wa Awamiyya katika mkoa wa Qatif nchini Saudi Arabia wamefanya maandamano makubwa ya kulalamikia kutiwa mbaroni kwa Ayatullah Namr Baqir Aali Namr mwanazuoni mashuhuri wa Kishia nchini humo.
Waandamanaji walimwagika mitaani na kushiriki kwenye maandamano makubwa mara tu baada ya kuenea habari za kutiwa mbaroni mwanazuoni huyo, ambapo watu watatu waliuawa kwa kupigwa risasi na askari usalama na wengine kudhaa kujeruhiwa.
Askari usalama wa Saudi Arabia walimtia mbaroni mwanazuoni huyo hapo jana alasiri baada ya kutumia nguvu na kumjeruhi.
Askari hao walifyatulia risasi gari lililokuwa limembeba mwanazuoni huyo na kulipelekea kugonga ukuta wa moja ya nyumba zilizokuwa karibu na kisha kumkamata. 1048191
captcha