IQNA

Idara ya kidini ya Karbala yataka kulindwa maeneo matakatifu nchini Syria

16:32 - July 29, 2012
Habari ID: 2380102
Idara ya kidini ya Karbala pamoja na Haram mbili za Imam Hussein na Abul Fadhl (as) zimeitaka serikali ya Iraq kuingilia kati mara moja na kufanya juhudi za kulindwa maeneo matakatifu nchini Syria.
Kwa mujibu wa gazeti la ar-Rai al-Aam, Idara hizo zimeitaka serikali ya Baghdad kutumia ushawishi wake wote kwa ajili ya kuzitaka pande husika kulinda na kuheshimu maeneo hayo na hasa Haram ya Bibi Zainab (as) dhidi ya hujuma ya makundi ya kigaidi yanayopigana kuangusha serikali halali ya Rais Bashar al-Asad.
Kwa mujibu wa taarifa za idara hizo, pande zote zinazopigana nchini Syria zinapasa kujiepusha na vitendo vyovyote vinavyodhuru na kuharibia heshima maeneo hayo.
Taarifa hiyo pia imezikosoa baadhi ya nchi za Kiarabu zinazochochea na kuyapa silaha makundi ya kigaidi kwa ajili ya kudumisha mapigano haribifu na kuchochea vita vya kikabila na kimadhehebu nchini Syria.
Makundi ya kigaidi yametishia kulipua Haram ya Bibi Zainab mjini Damascus. 1064694
captcha