Ujumbe huo umewasilishwa na balozi wa Saudia nchini Iran Mohammad al Kilabi wakati alipokutana na Mkuu wa Ofisi ya Rais Rahim Mashai.
Balozi huyo amesema Mfalme Abdullah ameitisha ‘Kikao Kisicho cha Kawaida cha Mshikamano wa Kiislamu ili kuhakikisha kuna umoja katika kipindi hiki nyeti ambapo Waislamu wanakumbwa na mifarakano na fitina.’
Kikao hicho kinatazamiwa kujadili masuala muhimu yanayohusu umma wa Kiislamu. Imedokezwa kuwa kadhia ya Syria itatawala kikao hicho huku kukiwa na mashinikizo dhidi ya Damascus.
Waislamu wengi duniani wanaamini kuwa kadhia ya Palestina hasa kuukomboa mji wa Quds unaokaliwa kwa mabavu na Israel ndio suala linalopaswa kupewa umuhimu na nchi za Kiislamu.
1071035